Tanzania: Matokeo ya Mtihani
1 Machi 2012Matangazo
Pamoja na kuonesha kuwa asilimia 53.59 ya wanafunzi 426,314 waliofanya mtihani huo wamefaulu, wengine kiasi cha 3,301 wamefutiwa matokeo kutokana na vitendo vya udanganyifu.
Kutokana na matokeo hayo Sudi Mnette amezungumza na Meneja wa Habari na Utetezi kutoka Haki Elimu nchini humo, Nyanda Shuhe ambae imetoa tathmini ya shirikia hilo na kutaka kila upande kuanzia mzazi kushiriki katika kuboresha kiwango cha elimu. Kusikiliza mahojiano hayo bonyeza alama za spika ya masikioni hapo chini.
Mwandishi: Sudi Mnette
Mhariri: Mohammed Khelef