1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

TALLLINN: Uchaguzi wa bunge wafanywa nchini Estonia

4 Machi 2007
https://p.dw.com/p/CCMY

Wapiga kura nchini Estonia hii leo wanachagua bunge jipya.Huu ni uchaguzi wa kwanza kufanywa Estonia tangu nchi hiyo kuingia katika Umoja wa Ulaya mwaka 2004.Kwa mujibu wa uchunguzi wa maoni wa hivi karibuni,“Chama cha Mageuzi“ cha Waziri Mkuu Andrus Ansip cha sera za wastani na pia “Chama cha Kati“ cha mrengo wa kushoto vina nafasi nzuri ya kujikingia kura nyingi.Safari hii,wapiga kura wameweza vile vile kupiga kura zao mapema juma hili,kwa kutumia mtandao wa Internet.