Watu zaidi ya 120 wamekufa kutokana na tetemeko la ardhi kwenye mpaka wa Iran na Irak. Waziri mkuu wa Lebanon asema atarejea nchini humo katika siku chache zijazo. Watu 34 wamekufa kutokana na ajali ya treni nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Shirika la kutetea haki za binadamu duniani latoa madai mazito dhidi ya serikali ya Syria.