Serikali ya Rwanda yatoa maoni yake kuhusu Kukamatwa kwa waasi wa FDLR nchini Ujerumani
18 Novemba 2009Matangazo
Kiongozi wa kundi hilo, Ignace Murwanashaka mwenye umri wa miaka 46 alikamatwa katika mji wa Karlsruhe, huku naibu wake Straton Musoni mwenye umri wa miaka 48 akikamatwa katika mji wa Stuttgart hapa Ujerumani. Serikali ya Rwanda imesema kukamatwa kwa wawili hao ni hatua nzuri katika kuhakikisha haki inatekelezwa kwa waathiriwa wa maovu hayo nchini Rwanda na Jamuhuri ya kidemokrasi ya Kongo.
Kutoka mji wa Kigali mwandishi wetu Daniel Gakuba anafuatilia tukio hilo na hii hapa ripoti yake kamili.
Mtayarishaji:Daniel Gakuba
Mpitiaji:Jane Nyingi