1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Senegal yaliokoa bara la Afrika kombe la dunia

Sekione Kitojo
20 Juni 2018

Senegal imedhihirisha kuwa muokozi wa bara la Afrika katika fainali hizi za kombe la dunia jana Junamme ukiondoa ushindi wao dhidi  ya  Poland inakuwa vipigo mara tano kwa wawakilishi wa bara hilo nchini Urusi.

https://p.dw.com/p/2zuZm
FIFA Fußball-WM 2018 in Russland | Polen vs. Senegal
Picha: Getty Images/C. Ivill

Baada  ya  Nigeria  na  Algeria  ambazo zote  zilifikia  awamu  ya  mtoano miaka  minne  iliyopita, baada  ya Ghana  kufikia  robo  fainali  mwaka  2010, tayari  inaonekana  kama mwaka  2018 kuwa  ni  hatua  moja  nyuma  kwa  bara  la  Afrika katika  medani  ya  juu  kabisa ya soka duniani.

WM 2018 Russland | Robert Lewandowski
Mshambuliaji wa Poland robert Lewandowski akiwa ameduwaa baad ya kipigo dhidi ya SenegalPicha: imago/ZUMA Press/A. Surma

Kufuatia  hamasa  kubwa  ya  kuwakilishwa  kwa  mara  ya  kwanza katika  fainali  hizi  tangu  mwaka  1990, Mafaraoh wamejikuta wakiutumbulia  macho mlango  wa  kutoka  baada  ya  siku  sita  za mashindano  haya.

Kikosi  cha  Hector Cuper  kimeathirika  na  matatizo  ya  kiafya  ya Mohamed Salah, ambaye  hakushiriki  katika  kipigo  cha  bao  1-0 dhidi  ya  Uruguay mjini  Yekaterinburg.

Jana  Jumanne(19.06.2018), Salah  alirejea  katika  kikosi  hicho lakini  alishindwa  kuzuwia Misri  kupokea  kipigo  kingine mara  hii mabao 3-1  dhidi  ya  Urusi mjini  Saint Petersburg,  mkwaju  wake wa  penalti katika  dakika  za  mwisho ukiwa  kama  la  kufutia machozi.

Russland WM 2018 Russland gegen Ägypten
Mohamed Salah akipachika bao la penalti ambalo halikuisaidia Misri dhidi ya wenyeji wa kombe la dunia Urusi katika kipigo cha mabao 3-1Picha: Reuters/P. Olivares

"Ni  vigumu mno kutambua  kile ambacho  kingetokea ( iwapo asingekuwa  majeruhi) lakini  tunafahamu  uwezo  wake," alisema kocha  Cuper.

Misri  bado  haijashinda  mchezo  wake  katika  fainali  za  kombe  la dunia  katika  mara  sita  za  kujaribu. Ni Honduras pekee ambayo imejaribu  mara  tisa ilicheza  michezo  mingi  zaidi  katika  fainali  za kombe  la  dunia  bila  ya  kupata  ushindi wowote, na  Mafaraoh wanafahamu  kwamba  sare  kwa  Uruguay dhidi  ya  Saudi Arabia siku  ya  Jumatano  jioni itashuhudia wakienguliwa  katika mashindano  haya.

Morocco  waishiwa  nguvu

Kikosi  cha  Herve Renard  wa  Morocco  hakikuwahi  kufungwa  bao hata  moja  wakati  wa  kufuzu  kucheza  katika  fainali  hizi  katika kundi  lao barani  Afrika. Na ilikuwa  bao  la  dakika  za  mwisho  la kujifunga la Aziz Bouhaddouz lililosababisha  kipigo  cha  bao 1-0 dhidi  ya  Iran katika  mchezo  wao  wa  ufunguzi.

Marokko - Iran - FIFA WM 2018 - Gruppe B - St. Petersburg Stadium
Mashabiki wa Iran wakati wa mchezo dhidi ya MoroccoPicha: Reuters/M. Dalder

Walianza  mchezo  huo  vizuri  sana , wakianza  kwa  kuwabana wachezaji  wa Iran  wakiwa  langoni  mwao, (pressing), wakati Amine Harit  akicheza  vizuri sana.  Lakini  waliishiwa  nguvu  na wamebakiwa  na  mchezo  dhidi  ya  Ureno  ya  Cristiano Ronaldo na  Uhispania  kujaribu  kuokoa  kampeni  yao, hali  ambayo  ni ngumu.

"Hatuna  muda  wa  kusikitika," amesema  Renard, na  hata  kama Morocco  itayaaga  mashindano  na  mapema, matumaini  ni kwamba  hii  itakuwa eneo  la  kujifunza kwa  wachezaji  chipukizi wenye  kipaji.

Herve Renard Trainer
Kocha wa Morocco Herve RenardPicha: Picture-Alliance/dpa/EPA/STR

Kikosi  cha  tai wa  kijani  cha  kocha  Gernot Rohr walifanya  vibaya wakati  walipoanza  kampei  kwa  kipigo  cha  mabao 2-0 dhidi  ya Croatia mjini  Kaliningrad  katika  kundi  gumu, ambalo  pia  lina  timu za  Argentina na  Iceland.

Goli  la  kujifunga  la  Oghenekaro Etebo  na  penalti  iliyopigwa  na Luka Modric iliifanya  Nigeria  hata  kutotambulika  tena kutoka  timu ile  iliyofungwa  na  Ufaransa  katika  awamu  ya  timu  16  zilizosalia katika  fainali  za  kombe  la  dunia  miaka  minne  iliyopita.

"Baadhi  ya  nyakati  tulikuwa  hatujielewi kunapotokea  mipira  ya adhabu lakini  tutaifanyia  kazi,"  amesema Rohr, ambaye  timu  yake itapabambana  na  Iceland.

Kocha  wa  Tunisia Nabil Maaloul  amesisitiza  kwa  kujiamini  kabla ya  fainali  hizi  za  kombe  la  dunia kwamba  kikosi  chake  kitafuzu kuingia  katika  awamu  ya  mtoano  kutoka  katika  kundi  ambalo lina  timu  za  Ubelgiji  na  Uingereza na  karibu  wangekilazimisha kikosi  cha  kocha  Gareth  Southgate  kutoka  sare mjini  Volgograd katika  mchezo  wao  wa  kwanza.

England Training und Pressekonferenz - Tottenham Hotspur Football Club Trainingsgelände
Kocha wa Uingereza Gareth SouthgatePicha: picture-alliance/D.Klein

Walirejea  mchezoni  baada  ya  kukubali  bao la  mapema  na walimpoteza  mlinda  mlango Mouez hassen  kutokana  na  kuumia, na  wakasawazisha kwa  mkwaju  wa  penalti  wa  Ferjani Sassi.

Baada  ya  kuona  timu  nyingine  za  Afrika  zikipata  kibarua kigumu, Senegal ilifanya  wajibu  wake  kwa  kupambana  kiume  na kutoka  na ushindi  wa  mabao 2-1 dhidi  ya  Poland jana  Jumanne (19.06.2018) katika  kundi  H.

Mwandishi: Sekione  Kitojo