NOUADHIBOU.Wahamiaji wasio halali kurejeshwa makwao
13 Februari 2007Matangazo
Meli iliyokuwa imewabeba watu 370 wanaodhaniwa kuwa ni wahamiaji wasio halali wenye asili ya kiafrika na kiashia imetia nanga katika bandari ya Nouadhibou nchini Mauritania.
Inaaminika kuwa meli hiyo ilikuwa inaelekea katika visiwa vya Canary nchini Uhispania wakati ilipoharibika.
Maafisa wa usalama wa Uhispania waliikamata meli hiyo wiki moja iliyopita.
Watu hao watarudishwa makwao kwa mujibu wa taarifa za utawala wa Uhispania.