1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Netanyahu aionya Iran katika mkutano wa usalama Munich

Sekione Kitojo
18 Februari 2018

Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema leo Jumapili (18.02.2018) kuwa nchi yake itachukua hatua dhidi ya Iran,na sio tu washirika wake wa mashariki ya kati, akirudia kwamba Tehran ni kitisho kikubwa kwa dunia.

https://p.dw.com/p/2st7Y
München MSC 2018 | israelischer Ministerpräsident Benjamin Netanjahu
Picha: picture-alliance/dpa/MSC 2018/L. Preiss

Akishikilia  kipande cha kile alichosema  kuwa  ni  ndege  ya  Iran isiyokuwa  na  rubani baada  ya  kuingia  katika  anga  ya  Israel mapema  mwezi  huu, Netanyahu ameuambia  mkutano  wa  usalama  mjini Munich, kwamba "Israel  haitauruhusu  utawala  huo  kuweka  kitanzi  cha ugaidi  katika  shingo.

München MSC 2018 | israelischer Ministerpräsident Benjamin Netanjahu
Waziri mkuu wa Israel akihutubia mkutano wa usalama mjini MunichPicha: picture alliance/dpa/S. Hoppe

"Tunachukua  hatua iwapo itakuwa muhimu sio tu dhidi ya washirika wa Iran lakini  dhidi  ya  Iran yenyewe ,"  alisema.

Akiuhutubia  mkutano  wa  usalama  mjini  Munich kwa mara  ya kwanza, Netanyahu amewataka maafisa  wa   Marekani  na Ulaya waliokusanyika  pamoja  na  wanadiplomasia  kupambana  na  Iran haraka, akionesha  ramani inayoonesha  kile alichosema  kuwa  ni uwepo  wa  Iran  unaoongezeka  katika  mashariki  ya  kati.

Amesema  Iran inaongeza  nguvu  zake wakati  muungano unaoongozwa  na  Marekani  dhidi ya  kundi  linalojiita  Dola  la Kiislamu  nchini  Iraq na Syria  unakomboa maeneo kutoka  kwa wanamgambo  hao.

Himaya ya Iran

"Kitu cha  kusikitisha ni  kwamba  wakati IS inapotea na  Iran inachukua  maeneo  yake, inajaribu  kujenga  himaya inayoendelea ikizunguka  eneo  la  mashariki  ya  kati  kutoka  kusini  nchini Yemen  lakini  pia  ikijaribu  kujenga  daraja  la  ardhini  kutoka  Iran kwenda  Iraq , Syria , Lebanon  na  Gaza," Netanyahu  alisema. "Hizi ni  hatua  za hatari  kwa  eneo  letu."

Syrien Reste einer Rakete in Quneitra
Mabaki ya kombora nchini SyriaPicha: Reuters/A. al Faqir

Wasiwasi  uliongezeka mnamo Februari  10 wakati  kombora la kupambana  na  ndege  za  kivita  lilipoiangusha  ndege  ya  kivita  ya Israel ikirejea  kutoka  kufanya  mashambulizi katika maeneo yanayodhibitiwa  na  Iran  nchini  Syria. Hayo  ni  mapambano halisi hadi sasa  kufanywa  na  Israel  na  majeshi  yanayoungwa  mkono na  Iran yaliyoko  katika  mpaka.

Wakati huo  huo msemaji wa  waziri  mkuu  wa Poland Mateusz Morawiecki, ameamua  kutotilia maanani maneno  ya  waziri  mkuu yanayobadilisha  mtazamo  wa  Poland  wa ushirika katika mauaji  ya Wayahudi , Holocaust  na kuwa ni madai  ya "Wayahudi wakosaji" kwa  kusema  ni matamshi  ya kukaribisha  mjadala wa  wazi  juu  ya uhalifu  wa  vita  vikuu  vya  pili vya dunia  dhidi  ya  Wayahudi.

Wanasiasa  wa  Israel wamemshutumu  waziri  mkuu  wa  Poland kwa  chuki  dhidi  ya  Wayahudi  kufuatia  matamshi  yake  hayo jana Jumamosi (17.02.2018) katika  mkutano wa  usalama  mjini  Munich, akifungua  ukurasa  mpya  katika  mzozo wa hasira kuhusiana  na sheria mpya ya Poland inayopita  marufuku  baadhi  ya  hotuba za mauaji  ya  Holocaust.

München MSC 2018 | polnischer Ministerpräsident Mateusz Morawiecki
Waziri mkuu wa Poland Mateusz MorawieckiPicha: Getty Images/AFP/T. Kienzle

Msemaji  wa Morawiecki Joanna Kopcinska  amesema  leo Jumapili kwamba  maneno yake "yanapaswa  kutafsiriwa kama wito wa moyo mkunjufu kwa  ajili  ya  majadiliano  ya uhalifu  uliotendeka  dhidi ya Wayahudi wakati  wa  mauaji  ya  Holocaust, bila  kujadili utaifa wa wale  waliohusika. Taarifa  hiyo  iliyotolewa  kwa  lugha  ya Kipolish na  Kiingereza  imesema  matamshi  ya  Morawiecki " kwa vyovyote vile  hayakulenga  kukana  kuhusu  Holocaust."

Mwandishi: Sekione  Kitojo /rtre / ape

Mhariri: Lilian Mtono