1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Neil Armstrong afariki akiwa na umri wa miaka 82

26 Agosti 2012

Risala za rambirambi zinaendelea kutolewa kufutia kifo cha mtu wa kwanza kufika mwezini, mwana anga wa Marekani Neil Armstrong. Armstrong mwenye umri wa miaka 82, alifariki kutokana na matatizo ya moyo

https://p.dw.com/p/15wvK
FILE - In undated photo provided by NASA shows Neil Armstrong. The family of Neil Armstrong, the first man to walk on the moon, says he has died at age 82. A statement from the family says he died following complications resulting from cardiovascular procedures. It doesn't say where he died. Armstrong commanded the Apollo 11 spacecraft that landed on the moon July 20, 1969. He radioed back to Earth the historic news of "one giant leap for mankind." Armstrong and fellow astronaut Edwin "Buzz" Aldrin spent nearly three hours walking on the moon, collecting samples, conducting experiments and taking photographs. In all, 12 Americans walked on the moon from 1969 to 1972. (Foto:NASA/AP/dapd)
Mondlandung 1969 Neil ArmstrongPicha: NASA/dapd

Alikuwa kamanda wa kikosi cha safari ya Apollo 11 - pamoja na mwanaanga mwengine Buzz Aldrin. Mamilioni ya watu duniani kote waliweza kufuatilia kwenye televisheni  mnamo mwaka wa 1969, jinsi Armstrong alivyotua mwezini, umbali wa kilometa 400,000 kutoka kwenye sayari ya dunia.

Armstrong alisema kwamba alichokifanya, ilikuwa ni hatua fupi kwake kama binadamu mmoja, lakini ilikuwa ni hatua ndefu mbele, kwa binadamu wote duniani.
Armstrong alisema kwamba alichokifanya, ilikuwa ni hatua fupi kwake kama binadamu mmoja, lakini ilikuwa ni hatua ndefu mbele, kwa binadamu wote duniani.Picha: dapd

Armstrong alisema wakati huo kwamba alichokifanya, ilikuwa ni hatua fupi kwake kama binadamu mmoja, lakini ilikuwa ni hatua ndefu mbele, kwa binadamu wote duniani. Rais Barack Obama amemsifu mwanaanga huyo kuwa ni shujaa mkubwa kabisa wa Marekani ambae kamwe hatasahaulika.

Armstrong aliefariki kutokana na matatizo yaliyoyababishwa na maradhi ya moyo, baada ya kuifanyiwa upasuaji mapema mwezi huu, amesifiwa kwa utayarifu wa kuzikabili na kuzishinda changamoto zilizoonekana kutoweza kushindika. Rais Obama  aliyasema hayo wakati akiongoza  katika  kuwasilisha  rambirambi pamoja na mwanaanga Buzz Aldrin. Obama  amesema Armstrong alikuwa shujaa  wa  kweli.

Obama ameeleza kuwa wakati Armstrong na  wanaanga wenzake walipoanza safari yao katika  chombo cha  Apollo 11 mnamo mwaka wa 1969, waliyabeba matumaini ya taifa lote la Marekani. Wakati huo Obama alikuwa bado ana wiki mbili ili kutimiza umri wa miaka minane. Obama amesema, alipotembea kwenye eneo la mwezini kwa mara ya kwanza ,Neil Amstrong alianzisha kipindi cha mafanikio ya mwanadamu ambacho kamwe hakitasahaulika.

Picha za Armstrong akitembea mwezini zilionyeshwa moj kwa moja kwenye televisheni
Picha za Armstrong akitembea mwezini zilionyeshwa moj kwa moja kwenye televisheniPicha: NASA/Newsmakers

Mwanaanga  mwenzake, aliefuatana naye katika safari ya mwezini,Buzz Aldrin amesema ana uhakika kwamaba mamilioni ya watu wameungana naye katika kuomboleza kifo cha shujaa huyo wa Marekani. Buzz  Aldrin amesema atamkumbuka rafiki yake Armstrong kama jinsi wananchi wengine wa Marekani na wote duniani  watakavyomkumbuka mwanaanga huyo maarufu. Licha ya mafanikio yake makubwa yaliyotokana na safari  ya Apollo11 Armstrong hakuwa mpenda sifa wa vyombo vya habari na wakati wote alijaribu kuviepuka.

Armstrong hakuhisi kujitoa hadharani na kuvitumia vyombo vya  habari. Hayo ameyasema mwanaanga mwengine wa Marekani John Glenn aliekuwa Mmarekani wa kwanza kuizunguka sayari ya dunia. Wajerumani pia wametoa rambi rambi zao juu ya kifo cha mwanaanga huyo wa Marekani na wamesifu  mafanikio yake.

376713 01: Neil Armstrong steps into history July 20, 1969 by leaving the first human footprint on the surface of the moon. The 30th anniversary of the Apollo 11 landing on the moon is being commemorated on July 20, 1999. (Photo by NASA/Newsmakers)
Mondlandung 1969 Neil Armstrong FußabdruckPicha: NASA/dapd

Mkuu wa Shirika la utafiti wa anga la Ujerumani Profesa  Johann-Dietrich Wörner ameliambia shirika la  habari la dpa, kwamba  Armstrong aliyawakilisha mafanikio ya maalfu ya wahandisi   waliofanya  kazi kuifanikisha safari ya chombo cha Apollo 11.

Profesa huyo amesema  Armstrong alikuwa ishara kwa binadamu  ya kuonyesha kwamba juhudi zao za kutafiti mambo mapya zitahifadhiwa daima bila ya kujali iwapo utafiti huo utakuwa na faida kifedha.Profesa Wörner amesema Arsmstrong ataacha urithi utakaokumbukwa   daima duniani kote hata baada ya kifo chake.

Mwandishi: Abdu Mtullya/AFP
Mhariri: Bruce Amani