1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Matokeo yote kutangazwa vituoni

Sudi Mnette30 Septemba 2015

Tume ya Uchaguzi nchini Tanzania (NEC) imerejea msimamo wake wa kuhisabiwa kura zote zitakazopigwa kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu kwenye vituo vya kupigia kura, hatua iliyopokewa vyema na wadau wa uchaguzi.

https://p.dw.com/p/1GfvF

Pirikapirika za kuelekea uchaguzi mkuu wa tarehe 25 Oktoba zinazidi kushika kasi. Taarifa ya NEC iliyosema ni ya kusimamia haki katika mchakato huo inasema kwa sasa kura zote kuanzia udiwani, ubunge na Urais zitahesabiwa katika vituo vya kupiga kura na matokeo yake kutolewa hapo hapo katika kipindi kisichozidi masaa 72.

Sudi Mnette anazungumza na mchambuzi wa masuala ya kisiasa, Rutaraka Ate Junior, juu ya kauli hii ya NEC na maana yake kwa uchaguzi wa mwaka huu unaotajwa kuwa wa kihistoria.

Mwandishi: Sudi Mnette
Mhariri: Josephat Charo

Ruka sehemu inayofuata Gundua zaidi

Gundua zaidi