1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

NDJAMENA: Waasi wa Chad wapambana na vikosi vya serikali

26 Novemba 2006
https://p.dw.com/p/CCpG

Waasi mashariki mwa Chad,wameudhibiti mji mkuu wa eneo hilo,Abeche,baada ya kupigana vikali na vikosi vya serikali.Jeshi la serikali limesema limerudi nyuma ili kuzuia hasara ya maisha ya raia.Wanadiplomasia na mashirika yanayotoa misaada yameripoti juu ya uporaji katika mji wa Abeche ulio kilomita 160 kutoka mpaka wa Sudan.Mji huo ni kituo cha makundi mengi ya misaada yanayohudumia wakimbizi kutoka Chad na jimbo la magharibi la Sudan,Darfur.Serikali ya Chad inaituhumu Sudan kuwa inawasaidia waasi, lakini Khartoum inakanusha lawama hizo.Kwa upande wake Sudan,inaituhumu Chad kuwa inawasaidia waasi wenye asili ya Kiafrika katika jimbo la Darfur.