1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

NAIROBI: Andre achaguliwa mjumbe wa Umoja wa Ulaya nchini Somalia

19 Juni 2007
https://p.dw.com/p/CBqG

Umoja wa Ulaya umemteu mjumbe wake maalum nchini Somalia,kusaidia juhudi za kuleta hali ya utulivu katika taifa hilo lililovurugwa kwa vita.Mjumbe huyo ni Georges-Marc Andre aliewahi kuwa msimamizi wa shughuli za umoja huo,nchini Gambia na Burundi.Bw.Andre ambae ni Mbeligiji,atakuwa na makao yake katika mji mkuu wa Kenya,Nairobi.