Unapopita kumbi nyingi za starehe pamoja na vilabu vya pombe, ni jambo la kawaida kusikia muziki wa injili ukipigwa maeneo hayo. Swala hilo ni kinyume na ilivyokuwa siku za nyuma ambapo muziki wa injili ungeusikia tu kunakohubiriwa injili kwa mfano makanisani na mikutano ya injili. Je, ni kusema jamii imepoteza mwelekeo au ni swala la kuendana na wakati?