1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

MUZAFFARABAD: Pakistan yakumbuka wahanga wa tetemeko la ardhi

8 Oktoba 2006
https://p.dw.com/p/CD4u

Rais Pervez Musharraf wa Pakistan na wananchi wenzake wamebakia kimya kwa dakika moja kuadhimisha mwaka mmoja tangu kutokea tetemeko la ardhi lililoua kama watu 75,000 nchini humo.Zaidi ya watu milioni 3.5 wamepoteza makazi yao katika tetemeo hilo la ardhi lililokuwa na nguvu ya 7.6 katika Kipimo cha Richter.