1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mogadishu. Mapigano yanaendelea.

24 Desemba 2006
https://p.dw.com/p/CCgS

Mapigano nchini Somalia kati ya majeshi ya serikali yanayosaidiwa na majeshi ya Ethiopia na yale ya jeshi la mahakama za Kiislamu yameingia katika siku ya tano na kusambaa katika miji mingine miwili kiasi cah kilometa 300 kaskazini ya Mogadishu. Pande zote mbili zimesema kuwa mapigano yamekuwa makali katika miji ya Beledweyne na Bindiradley lakini hazikutoa maelezo zaidi kuhusu watu walioathirika.

Milio ya makombora pia imesikika karibu na Baidoa, mji ambao una makao rasmi ya serikali ya Somalia.

Mapigano yamezuka Jumatano wili iliyopita baada ya kumalizika kwa muda uliotolewa na mahakama za Kiislamu kwa majeshi ya Ethiopia kuondoka nchini humo. Ethiopia inakana kuwa majeshi yake yanahusika katika mapigano hayo, ikisema kuwa imetuma tu wataalamu wanaofundisha jeshi la nchi hiyo.

Majeshi ya mahakama za Kiislamu yanadhibiti mji mkuu Mogadishu na baadhi ya maeneo ya Somalia.