1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mogadishu. Mapigano bado yanaendelea.

23 Desemba 2006
https://p.dw.com/p/CCgv

Mapigano yanasemekana kuwa yanaendelea kati ya majeshi yanayounga mkono umoja wa mahakama za Kiislamu na majeshi ya serikali dhaifu ya mpito ya nchi hiyo.

Pia kuna ripoti kuwa Ethiopia imetuma vifaru na helikopta katika mstari wa mbele wa mapambano kusaidia majeshi ya serikali ya Somalia.

Muungano wa mahakama za Kiislamu tayari wanadhibiti mji mkuu Mogadishu na maeneo makubwa ya taifa hilo la pembe ya Afrika.

Pande zote mbili zimetangaza kutoa kipigo kwa upande mwingine baada ya siku kadha za mapigano, lakini hakuna taarifa za kuthibitisha madai hayo.

Mashirika ya kutoa misaada yamesema kuwa raia wanakimbia mapigano hayo na wanasema kuwa wana wasi wasi kuhusu wafanyakazi wao walioko katika maeneo hayo, ambao wanafanyakazi kuwasaidia wahanga baada ya wiki kadha za mvua kubwa.