1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mkutano wa G8 wamalizika

20 Mei 2012

Mkutano wa kilele wa nchi tajiri kiviwanda duniani G8 umemalizika huku viongozi wakiazimia kuzitumia njia zote za kukuza uchumi na mpango wa kubana matumizi kama suluhu ya kuutatua mzozo wa uchumi wa kanda ya Euro.

https://p.dw.com/p/14yt7
Leaders attend the family photo session at the G8 summit at Camp David, Maryland May 19, 2012. From L-R: European Commission President Jose Manuel Barroso, Russia's Prime Minister Dmitri Medvedev, Japan's Prime Minister Yoshihiko Noda, Canada's Prime Minister Stephen Harper, France's President Francois Hollande, U.S. President Barack Obama, German Chancellor Angela Merkel, Britain's Prime Minister David Cameron, Italy's Premier Mario Monti, and European Council President Herman Van Rompuy. REUTERS/Philippe Wojazer (UNITED STATES - Tags: BUSINESS POLITICS)
Auftakt G8-Gipfel in Camp David (USA)Picha: picture-alliance/dpa

Kwenye tamko lao la pamoja viongozi hao wamesema kuwa wamekubaliana kwa pamoja kuchukua hatua zinazohitajika kuinua na kuuimarisha uchumi wa nchi zao na kuudhibiti mtikisiko wa kifedha huku wakitambua kuwa hatua hizo hazitafanana kwa kila nchi.

Ujumbe huo wa jumla ambao ulisomwa na mwenyeji wa Mkutano huo wa siku mbili Rais wa Marekani Barack Obama, kwa kiasi fulani umerandana na mapendekezo yake kwamba mzozo wa uchumi wa kanda hiyo ambao kwa sasa unatishia hatma ya umoja huo wa nchi 17 unaweza kuuathiri pia uchumi wa nchi yake na kuvuruga fursa za kushinda uchaguzi wa Novemba.

epa03225964 Russian Prime Minister Dmitry Medvedev (C-R) speaks with German Chancellor Angela Merkel (C-L) during their meeting in the framework of the G8 Summit at at Camp David, the presidential retreat in Maryland, USA, 19 May 2012. The world's Group of Eight leading industrial nations (G8) meet at Camp David to discuss the European debt crisis, the global economy and security issues. EPA/MIKHAIL KLIMENTYEV/RIA NOVOSTI/KREMLIN POOL MANDATORY CREDIT MIKHAIL KLIMENTYEV/RIA NOVOSTI
Viongozi wa kundi la G8 wakiwa katika mkutano Camp DavidPicha: picture-alliance/dpa

Kanda ya euro yazidi kukabiliwa na matatizo

Kutokana na hali tata ya kisiasa na kiuchumi inayoikabili Ugiriki, kupungua kwa thamani ya fedha na mzozo wa madeni unaozidi kuchomoza Italia na Uhispania ambapo hisa zimekuwa zikishuka kwa kiwango kikubwa kila leo kundi hilo limekubaliana kuyatazama masuala hayo kwa utulivu zaidi na kurekebisha hali hiyo.

Kwenye hitimisho la mjadala wao wa kiuchumi, viongozi hao wametoa wito wa kuongezwa juhudi za kuutatua mzozo huo huku wakiunga mkono msimamo wa Ujerumani wa kubana matuimizi kwa nchi husika, kujiimarisha kiuchumi na kuongeza fursa za ajira.

Kuhusu uwezekano wa Ugiriki kujiuondoa kwenye kanda ya sarafu ya Euro, viongozi hao kwa pamoja wamesema kuwa nia yao ni kuiona nchi hiyo ikendelea kubaki kwenye umoja huo lakini pia wamesema wanaheshimu maamuzi ya nchi hiyo.

Wajadili pia Afghanistan na mashariki ya kati

Ni jambo lisilo la kawaida kwa mataiafa hayo tajiri kukaa na kuizunguumzia nchi ndogo kama hiyo, hofu ya kuwa hali ya mtafaruku wa kisiasa nchini humo unaweza kusababisha nchi hiyo kujiondoa kwenye kanda ya sarafu ya Euro kunawatia mashaka wakihofia kuporomoka kwa masoko na uchumi wa dunia kwa ujumla.

Wapiga kura nchiuni Ugiriki mwezi huu waliwaadhibu viongozi wa nchi hiyo wanaoungamkono mpango wa kubana matumizi kwa kutumia kura zao kwenye uchaguzi, na kisababisha yafanyaike marudio June 17 ambapo hadi sasa bado wingu la wasiwasi bado limetanda.

German Chancellor Angela Merkel, right, and Russian Prime Minister Dmitry Medvedev listen during the first meeting of the G-8 Summit Saturday, May 19, 2012 at Camp David, Md. (Foto:Charles Dharapak/AP/dapd)Bergmann/Bundesregierung/dapd
Kansela wa Ujerumani Angela Merkel akihudhuria mkutano wa kundi la G8 nchini MarekaniPicha: dapd

Mkutano huo pia ulijadili masuala mengine yakiwemo ya kisiasa ikiwa ni pamoja na ushirikiano wa kimataifa ikiwemo hali ilivyo nchini Afghanistan na Mashariki ya Kati.

Kundi la G8 linaundwa na nchi za Marekani, Ujerumani, Ufaransa, Canada, Italia, Uingereza, Urusi na Japan na mkutano wa safari hii umefanyika huko Camp David mjini Maryland nchini Marekani chini ya uenyeji wa Rais wa nchi hiyo Barack Obama.

Mwandishi: Stumai George

Mhariri: Sekione Kitojo