Mjumbe wa Umoja wa Mataifa azuru Kongo
12 Aprili 2010Matangazo
Bibi Wallstrom anatarajiwa kukutana badaye leo na waziri mkuu wa Kongo, Adolphe Muzito, na wanachama wengine wa serikali yake, na vile vile mashirika ya kiraia na yale yasiyo ya kiserikali ili kutathmini kwa pamoja kuhusu visa vya ubakaji dhidi ya wanawake na ukiukaji mwingine wa haki za binadamu nchini DRC. Ziara hiyo itampeleka pia kwenye majimbo ya kivu ya kusini na ya kaskazini.
Mtayarishaji: Josephat Charo
Mhariri: Othman Miraji