1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Misri yakabiliwa na mgawanyiko kuhusu hatma yake kisiasa

15 Desemba 2012

Wamisri leo Jumamosi (15.12.2012) wanapiga kura ya maoni kuhusu rasimu ya katiba yao mpya iliyoidhinishwa na wanasiasa wanaoyaunga mkono ya makundi ya Kiislamu kama njia ya kujitoa kutoka katika mzozo wa kisiasa

https://p.dw.com/p/172z4
A supporter of Egyptian President Mohamed Mursi and members of the Muslim Brotherhood put up posters that read "Yes to constitution" before Friday prayers during a rally at Rabaa El Adaweya Mosque square in Cairo December 14, 2012. Flag-waving supporters of Mursi staged a final rally on Friday before a divisive referendum on a new constitution that the Islamist leader hopes will bring an end to weeks of political crisis and street clashes. REUTERS/Amr Abdallah Dalsh (EGYPT - Tags: POLITICS CIVIL UNREST RELIGION)
Waandamanaji mitaani dhidi ya katiba mpyaPicha: Reuters

Makundi hayo ya vyama vya Kiislamu yanatupilia mbali tuhuma za wapinzani kuwa rasmu hiyo ya katiba ni chachu ya mgawanyiko zaidi katika taifa hilo kubwa la Kiarabu.

Upigaji kura umeanza leo katika mswada wa katiba ulioligawa taifa hilo, ambapo mzozo huo umekuwa kati ya waungaji mkono wa makundi ya Kiislamu yanayomuunga mkono rais Mohamed Mursi dhidi ya waliberali, wale wanaotaka kutenganishwa kwa dini na serikali pamoja na Wakristo katika mapambano ambayo mara kwa mara yamesababisha umwagikaji wa damu mjini Cairo pamoja na miji mingine.

Egyptian protesters shout slogans in front of burning cars set on fire during a demonstration calling for a 'No' vote in a referendum on a new constitution in the coastal city of Alexandria on December 14, 2012. Stone-throwing clashes broke out between Islamists and opposition supporters in Alexandria on the eve of the highly charged referendum, witnesses said. There was no immediate word on any casualties but witnesses told AFP street violence was continuing in Egypt's second-biggest city despite police efforts to restore order. AFP PHOTO/STR (Photo credit should read STR/AFP/Getty Images)
Maandamano ambayo yamekuwa na vuruguPicha: AFP/Getty Images

Upinzani unasema kuwa katiba hiyo inaelemea zaidi katika matakwa ya Kiislamu na inakanyaga haki za wachache. Waungaji mkono wa Mursi wanasema katiba hiyo inahitajika iwapo maendeleo yatafikiwa kuelekea demokrasia karibu miaka miwili baada ya kuanguka kwa utawala wa kijeshi wa Hosni Mubarak.

Mjini Alexandria jana Ijumaa(14.12.2012) hali ya wasi wasi ilitanda na kusambaa hadi kuwa mapambano ya mitaani baina ya makundi hasimu ambayo yamekuwa na marungu, visu, na panga.

A supporter of Egypt's President Mohamed Morsi and the Muslim Brotherhood holds a Koran, Islam's holy book, as he shouts slogans during a demonstration in the Nasser City district of Cairo on December 14, 2012. Weeks of protests and violent clashes between rival camps that left eight people dead last week have failed to dissuade Morsi from holding the referendum, which will be staggered over a week. AFP PHOTO/MARCO LONGARI (Photo credit should read MARCO LONGARI/AFP/Getty Images)
Waungaji mkono wa Mursi walijitokeza pia mjini CairoPicha: AFP/Getty Images

Magari yachomwa moto

Magari kadha yamechomwa moto na mhubiri mmoja wa dini ya Kiislamu ambaye alitoa wito kwa watu kupiga kura ya ndio kwa katiba hiyo alikwama ndani ya msikiti baada ya kuzingirwa na wafuasi wa upinzani ambao walikuwa na hasira.

Katika mji mkuu , Cairo, pande zote mbili zilifanya juhudi za wastani za mwisho kuwashawishi waungaji wao mkono.

Egyptian firefighters douse a burning car set on fire during a demonstration calling for a 'No' vote in a referendum on a new constitution in the coastal city of Alexandria on December 14, 2012. Stone-throwing clashes broke out between Islamists and opposition supporters in Alexandria on the eve of the highly charged referendum, witnesses said. There was no immediate word on any casualties but witnesses told AFP street violence was continuing in Egypt's second-biggest city despite police efforts to restore order. AFP PHOTO/STR (Photo credit should read STR/AFP/Getty Images)
Mapambano mjini Alexandria baina ya waandamanajiPicha: AFP/Getty Images

Makundi ya waungaji mkono vyama vya Kiislamu yakipunga bendera , yalijikusanya kwa amani katika msikiti mmoja mkubwa , baadhi wakiimba , "Uislamu, Uislamu" na "Tumekuja hapa kusema "NDIO", kwa katiba".

Waungaji mkono wa upinzani , ambao wametakiwa kupiga kura ya "HAPANA", na viongozi wao, walijikusanya nje ya ikulu ya Misri mjini Cairo.

Jengo hilo linaendelea kuzingirwa na polisi, wanajeshi na vifaru vya jeshi baada ya mapambano ya mitaani kusababisha kiasi ya watu wanane kuuwawa mapema mwezi huu katika ghasia zilizosababishwa na uamuzi wa rais Mursi kujipa madaraka makubwa ili kuweza kupitishwa kwa rasmu ya katiba mpya.

Wakati giza linaanza kutanda , kulionekana tu watu ambao walikuwa wakiangalia hali ya mambo pamoja na wachuuzi katika eneo hilo badala ya waandamanaji.

Protesters opposing Egyptian President Mohamed Mursi sit around a fire to warm themselves up at Tahrir Square in Cairo December 14, 2012. Supporters and opponents of Mursi stage final rallies on Friday before a divisive referendum on a new constitution championed by the Islamist leader as a way out of the worst crisis since the fall of Hosni Mubarak. REUTERS/Khaled Abdullah (EGYPT - Tags: POLITICS CIVIL UNREST)
Waandamanaji mjini CairoPicha: Reuters

Mursi ashambuliwa

Mwanamke mmoja alikuwa akiliambia kundi la watu kupitia kipaza sauti, akitoa matusi kwa Mursi, lakini wengi wa watu waliokuwa wakimsikiliza hawakuonekana kujali anayosema na kuendelea kunywa chai ama kupiga picha mbele ya kifaru.

"Simpendi Mursi," amesema Moustafa Ahmed , mwenye umri wa miaka 25, na mwalimu. "Lakini sijaamua jinsi nitakavyopiga kura , kwa hiyo nimeamua kuja hapa kusikiliza waandamanaji na kuzungumza nao kwa mara ya mwisho."

Mwandishi: Sekione Kitojo / rtre

Mhariri: Stumai George