Miripuko yatikisa Msikiti Mwekundu
7 Julai 2007Matangazo
Hapo awali,miripuko miwili iliutikisa msikiti huo huku vikosi vya usalama vikizidi kuwazingira wale waliojificha ndani ya msikiti.Maalim mmojawapo amesema,yeye na wafuasi wake wapo tayari kufa badala ya kusalim amri.
Inasemekana kuwa katika jengo hilo,kuna kama watu 300 ikiwa ni mchanganyiko wa wanaume,wanawake na watoto. Wakati huo huo,mashhehe wengine hii leo wanatazamia kuzungumza na maalim huyo,ili watoto walio katika msikiti huo wapate kuachiliwa huru.
Hadi hivi sasa watu 19 wameuawa katika mapigano yaliyozuka kati ya vikosi vya serikali na wanamgambo waliojificha nsikitini.Viongozi wa Msikiti Mwekundu wanataka sheria kali za Kiislamu zitumike kote nchini Pakistan.