1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Miaka 72 ya mauaji ya Holocaust

Mohammed Abdulrahman27 Januari 2017

Ijumaa ni suku ya kimataifa ya kuwakumbuka wahanga wa mauaji ya Kimbari-Holocaust, yaliofanywa na utawala wa Wanazi wakati wa vita vya pili vya Dunia. Wakati wa utawala  huo wa, Adolf Hitler, watu milioni 1.1 waliuwawa.

https://p.dw.com/p/2WVu7
Deutschland Holocaust Gedenkstunde des deutschen Bundestages
Picha: Reuters/A. Schmidt

Bunge la Ujerumani Bundestag, lilipanga kuwa na hafla ya saa moja kuwakumbuka  mamilioni ya wahanga wa utawala wa wanazi . Pia hafla  kama hiyo, iliandaliwa na  sehemu kubwa ya mabunge ya Mikoa ya Shirikisho . Wabunge wa bunge la Mkoa wa Bavaria wamelizuru baraza la Senete la bunge la Jamhuri ya Czech, mjini Prague na kuweka shada la maua mahala pa kumbukumbu katika mji wa Litomerice.

Kiasi ya watu 4,500 waliuwawa katika mji huo ulioko kaskazini mwa Prague, palipokuweko kambi ya wahanga ya Flossenbuerg katika mpaka wa Bavaria kuelekea Jamhuri ya Czech.

Sambamba na hayo wanakumbukwa wahanga wa mpango wa mauaji wa Hitler, ambapo walemavu na wagonjwa jumla ya watu 300,000 waliuawa, wakionekana kama watu wasio na maana katika jamii, wahanga ambao kwa muda mrefu walisahauliwa.

Zaidi ya watu 70,000 waliuwawa kwa gesi ya sumu katika  maeneo sita yaliokuwa yakidhibitiwa na Ujerumani baina ya  Januari 1940 na  Agosti 1941.

Deutschland Holocaust Gedenken zum 72. Jahrestag der Befreiung von Auschwitz
Kumbukumbu ya mauaji ya Holocaust ya Ujerumani kwenye maadhimisho ya miaka 72Picha: picture-alliance/dpa/A. Grygiel

 Katika hafla ya leo bungeni mjini Berlin iliohudhuriwa pia na Kansela Angela Merkel, Spika wa bunge la Ujerumani, Norbert Lammmert, alisema  mpango huo ulikuwa wa kwanza ambapo ilitumiwa gesi ya sumu kwa wale walioonekana hawana maana kuishi na kugeuka kuwa majaribio kuelekea mauaji ya kimbari - Holocaust dhidi ya Wayahudi.

Mnamo mwaka 1996 Rais wa Ujerumani wakati huo, Roman Herzog, alipendekeza Januari 27, siku ya  kukombolewa kambi ya Auschwitz, kuwa siku ya Ujerumani kuwakumbuka wahanga wa  utawala wa Wanazi na tangu wakati huo inafanyika kila mwaka.

Polen Auschwitz Holocaust Gedenktag
Maadhimisho ya nchini Poland ya mauaji ya Holocaust Picha: picture-alliance/AP Photo/C. Sokolowski

Mwaka 2005 Umoja wa Mataifa, ukaitangaza Januari 27 kuwa Siku ya Kimataifa kuwakumbuka wahanga wa mauaji ya Kimbari ya Holocaust, wakati wa vita vikuu vya pili vya Dunia- siku a majeshi ya Urusi yalipoikomboa kambi ya mateso ya Auschwitz nchini Poland  1945.

Miongoni mwa  Wayahudi milioni 6 waliouwawa, milioni moja walikufa katika kambi ya Auschwitz, wengi katika kumbi za gesi, sambamba na maelfu ya wengine wakiwemo Wapoland, watu wa jamii ya Waroma, pamoja na Warusi waliokamatwa kama wafungwa wa kivita.

Mwandishi. Mohammed Abdul-rahman, dpa, afp

Mhariri:Yusuf Saumu