Miaka 10 tangu shambulio la 9/11
11 Septemba 2011Raia nchini humo wanajitayarisha kwa maadhimisho ya siku hii.Katika hotuba yake ya kila wiki, Rais Barack Obama hapo jana alisema kuwa muongo mmoja baadaye Marekani imekuwa na nguvu zaidi, huku kundi la kigaidi la Al Qaeda linaelekea kushindwa.
Aligusia hususan kuuliwa kwa kiongozi mkuu wa kundi hilo, Osama bin laden mapema mwaka huu. Rais wa zamani nchini humo, George.W. Bush, aliyekuwa uongozini wakati wa shambulio hilo, alihudhuria sherehe za kuweka shada la maua katika wizara ya ulinzi, Pentagon.
Bush alieleza masikitiko yake kwa familia na marafiki za wahanga takriban 3000.
Maadhimisho kadhaa yamepangwa kote nchini hii leo katika kumbukumbu ya siku hii. Wakati huo huo, matayarisho ya kumbukumbu hiyo yamegubikwa na kitisho cha onyo kwa umma kilichotolewa na maafisa wa usalama nchini humo, kinachoaminika kutokana na uwezekano wa mpango wa mashambulio dhidi ya mji wa New York na ama Washington D.C.
Mwandishi: Maryam Abdalla/rtre, ape, afpe, tv
Mhariri: Kitojo Sekione