Kansela wa Ujerumani, Angela Merkel, leo hii anaendelea ziara yake ya siku nne katika Mashariki ya Kati. Baada ya kuzitembelea Misri na Saudi-Arabia, leo Bi Merkel aliwasili nchini Umoja wa Falme za Kiarabu. Pamoja na kuzungumzia mkakati wa kutafuta suluhisho kati ya Wapalestina na Waisraeli, Angela Merkel pia anafanya mazungumzo juu ya kurahisisha biashara kati ya eneo hili na Umoja wa Ulaya.