Merkel na Bush kutafuta suluhisho la kidiplomasia
12 Novemba 2007Matangazo
Katika mkutano wao pamoja na waandishi wa habari,Merkel na Bush waliahidi kuendelea kutafuta suluhisho la kidplomasia kuhusu mgogoro wa mradi wa nyuklia wa Iran.
Merkel akasema,ataunga mkono duru nyingine ya vikwazo dhidi ya Iran ikiwa Iran itaendelea kupinga mwito wa jumuiya ya kimataifa kusitisha harakati za kurutubisha madini ya uranium.
Kansela Merkel akaongezea kuwa walijadiliana pia kwa kirefu,mkutano wa hali ya hewa utakaofanywa Bali nchini Indonesia na anaamini mkutano huo una nafasi nzuri ya kufanikiwa.