1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mawaziri wa ulinzi watathimini mapambano dhidi ya IS

Sekione Kitojo
26 Oktoba 2016

Mawaziri wa ulinzi wa mataifa yanayounda muungano unaoongozwa na Marekani dhidi ya kundi la Dola la Kiislamu walikutana mjini Paris jana (25.10.2016)kutathmini vita dhidi ya kundi hilo.

https://p.dw.com/p/2RiOj
Paris | Treffen der Verteidigungsminister der Anti-IS-Koalition in Paris - Francois Hollande
Rais Francois Hollande akihutubia mkutano wa muungano unaoongozwa na Marekani dhidi ya kundi la IS.Picha: picture-alliance/dpa/C. Platiau

Mawaziri  hao wa  ulinzi  walikuwa  wanakutana  mjini Paris jana, kutathmini hali  ya  vita  dhidi  ya kundi  hilo baada ya zaidi  ya  miaka miwili ya  mashambulio ya anga,mafunzo pamoja na ushauri  kwa wanajeshi  wanaopambana  katika  vita  vya kuukomboa  mji wa  Mosul. 

Waziri  wa  ulinzi  wa  Ufaransa  Jean-Yves Le Drian alikuwa akikutana  na  mawaziri  wenzake  pamoja  na  waziri  wa  ulinzi  wa Marekani  Ashton Carter katika  kutathmini  kazi  iliyofanywa  na muungano  huo  katika  muda  wa  miaka  miwili  iliyopita  dhidi  ya kundi  la  Dola  la  Kiislamu. Mbali  na  kuratibu  msaada  wao  kwa majeshi  yanayokaribia  kuukomboa  mji  wa  Mosul , mawaziri  hao walijadili  pia  hali  ya  kampeni  kama  hiyo  upande  wa  Syria  na kusema  wanatayarisha   mpango  kwa  ajili  ya  kuutenga  mji  wa Raqa.

Paris - Verteidigungsminister der Anti-IS-Koalition beraten in Paris
Wajumbe wa muungano unaoongozwa na Marekani katika vita dhidi ya kundi la ISPicha: REUTERS/C. Platiau

Ufaransa  ina nia  ya  kutaka  kuutenga  mji  wa  Raqa , ambako wapiganaji  wa  IS  wapatao  3,000  hadi  4,000  ikiwa  ni  pamoja na  jumla  ya   raia  karibu  300  wa  Ufaransa   ambao  kurejea kwao  nchini  Ufaransa  wakati  Dola  la  Kiislamu  litakapoporomoka ni hali  inayofikiriwa  kuwa  kitisho  kikubwa  cha  kitaifa.

Wakati  mawaziri  hao  wakikutana, rais  wa  Ufaransa  Francois Hollande  ameonya  kwamba , kukombolewa  kwa  mji    wa  Mosul sio  mwisho  wa  mapambano  dhidi  ya  kundi  hilo.

"Kile  kilichopo  sasa  ni  hali  ya  baadaye  ya  kisiasa  ya  mji  huo, jimbo  hilo  na  Iraq, na  nchi  zilizomo  katika  muungano pia zinapaswa  kusaidia katika  utekelezaji  katika  kuiongoza serikali ambayo  itajumuisha  makundi  yote katika  mji  wa  Mosul. Makabila yote  pamoja  na  makundi  ya  kidini  yatawakilishwa. Na  amani iliyotarajiwa  itakuwapo."

München Sicherheitskonferenz Jean-Yves Le Drian
Waziri wa ulinzi wa Ufaransa Jean-Yves Le DrianPicha: Reuters/M. Dalder

IS yaendelea  kupambana 

Likitaka  kuondoa  mtazamo  kutoka  kampeni  ya  mapambano  dhidi ya  mji  wa  Mosul ,  kundi  la  IS  lilifanya  mashambulio  katika  mji wa  kaskazini  wa  Kirkuk  na  mji  wa  magharibi  wa  Rutba  katika siku  za  hivi  karibuni.

Wapiganaji  hao  wa  Jihadi  walikamata  vitongoji  viwili  katika  mji wa  Rutba , lakini  maafisa  wamesema  kwamba  tangu  jana Jumanne  vitongoji  hivyo  vimerejeshwa katika udhibiti wa  majeshi  ya  serikali.

Maafisa  waandamizi  wa  Marekani  na  Iraq  wameripoti  kwamba viongozi  wa  IS  tayari  wanajaribu  kuondoka  kutoka  Mosul  na kwenda  katika  mamlaka  ya  kikhalifa  upande  wa  Syria.

Irak Region Mossul Peschmerga Kämpfer
Wanajeshi wa Iraq wakipambana na wapiganaji wa IS karibu na mji wa MosulPicha: Reuters/A. Jadallah

Lakini  afisa   ambaye  yuko  karibu  an  waziri  wa  ulinzi  wa Ufaransa  Le Drian  amesema  wapiganaji  mia  chache  wa  kundi  la IS  hivi  karibuni  walihamia katika  eneo  la  maigano, wakiimarisha nguvu ya wenzao  wapatao 3,000  hadi  5,000  wanaopambana kuulinda  mji  wa  Mosul. Kundi  la  IS  limeonesha  uwezo  mkubwa wa  mapambano , na  pia  kurejea  nyuma  wakati  wakishambuliwa kwa  nguvu.

Lakini  madai  yao  ya  kutaka  kuunda  mamlaka  ya  Kikhalifa yakikosa  uhalali  kila  wakati  wanapopoteza  eneo, IS  imekuwa ikileta  upinzani  mkubwa   katika  mapambano  katika  mji  wa  Mosul.

Mji  huo  ndipo  alipo  kiongozi  mkuu  wa  IS Abu bakr al-Baghdadi aliyetangaza  mamlaka  ya  Ukhalifa  katika  ardhi  iliyotekwa  kati  ya Syria  na  Iraq  mwezi  Juni , 2014  na  kukombolewa   kwa  mji  huo kutasababisha  mwisho  wa  kundi  hilo  kudhibiti  ardhi  katika upande  wa  Iraq.

Mwandishi:      Sekione  Kitojo  / afpe

Mhariri:  Iddi  Ssessenga