1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mawaziri wa Maji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakutana nchini Kenya kujadili Ziwa Viktoria

5 Septemba 2008

Nchini Kenya mawaziri wa maji kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wamefanya mkutano mjini Nairobi hii leo kujadilia makubaliano ya Mto Victoria.

https://p.dw.com/p/FCBH
Ziwa ViktoriaPicha: africa-photo

Azma ya kikao hicho ni kujadilia mbinu na mikakati ya matumizi ya maji ya mto huo ili kutimiza malengo ya maji na usafi chini ya mwamvuli wa malengo ya maendeleo ya Milenia ya Umoja wa mataifa.Mpango wa maendeleo ya Ziwa Victoria ulianzishwa mwaka 2001 na Jumuiya ya Afrika Mashariki.Mkutano huo unalenga kuratibisha matumizi ya maji ya Ziwa Victoria vilevile uwekezaji.

Kutoka Nairobi Alfred Kiti ameandaa taarifa ifuatayo.