Tuliyo nayo jioni hii: Vikosi vya jeshi la Syria vimezidi kusonga mbele huko Ghouta Mashariki. Jumla ya mashambulizi 950 yaliyowalenga Waislamu na taaasisi za Kiislamu, yaripotiwa nchini Ujerumani kwa mwaka uliopita. Iran, yasema hapawezi kuwa na mazungumzo yanayohusu mpango wa nchi hiyo wa makombora bila ya mataifa ya Magharibi kuteketeza silaha zake za nyuklia.