Marekani yasema Iran inazidi kuwasaidia wanamgambo wa kujitoa mhanga Iraq
25 Julai 2007Matangazo
Balozi huyo aliyasema hayo baada ya mkutano wake na maafisa wa Iran juu ya suala la usalama nchini Iraq, mkutano ambao ni watatu kati ya pande hizo mbili katika kipindi cha miongo mitatu iliyopita.
Balozi Crocker alisema Iran inachangia madhila makubwa wanayopata wananchi wa Iraq na ameitaka kueleza bayana nini inachokitaka.
Wakati huo huo watu 26 wamekufa na wengine 70 kujeruhiwa baada ya mshambuliaji wa kujitoa mhanga kujilipua katikati ya kundi la watu kwenye soko kuu la mji wa washia wa Hilla kusini mwa Iraq.
Mji huo uliyoko kiasi cha kilomita 100 kusini mwa Baghdad umekuwa ukikumbwa na mashambulio kadhaa ya kujitoa mhanga likiwemo la tarehe sita mwezi March ambapo watu 120 waliuawa.