1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mapambano makali yazuka Bangkok

15 Mei 2010

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon ametoa wito wa kusitisha matumizi ya nguvu nchini Thailand.

https://p.dw.com/p/NOeA
Thai soldiers move on anti-government protestors and others during an operation to secure an area near Lumpini Park in downtown bangkok, Thailand, Friday, May 14, 2010. Troops fired bullets and tear gas at anti-government protesters rioting near the U.S. and Japanese embassies as an army push to clear the streets sparked bloody clashes and turned central Bangkok into a virtual war zone. (AP Photo/Wason Waintchakorn)
Wanajeshi wakiwajongelea wapinzani wa serikali mjini Bangkok.Picha: AP

Wito huo umetolewa baada ya waandamanaji 10 kuuawa katika mapambano yaliyozuka kati ya wanajeshi na waandamanaji wa upande wa upinzani, wanaojulikana kama "mashati mekundu" pia. Ripoti zinasema jumla ya wale waliouawa, sasa imefikia 16 na zaidi ya watu 100 wamejeruhiwa, miongoni mwao wakiwemo raia watatu wa kigeni. Msemaji wa Ban Ki-moon amezihimiza pande zote mbili yaani serikali na waandamanaji hao warejee katika meza ya mazungumzo.

Anti-government protestors fire home made rockets at soldiers in an area near Lumpini Park in downtown bangkok, Thailand, Friday, May 14, 2010. Troops fired bullets and tear gas at anti-government protesters rioting near the U.S. and Japanese embassies as an army push to clear the streets sparked bloody clashes and turned central Bangkok into a virtual war zone. (AP Photo/Wason Waintchakorn)
Wapinzani wa serikali wakirusha kombora la kienyeji mjini Bangkok.Picha: AP

Machafuko yameendelea katika mji mkuu Bangkok, kwa siku ya tatu leo, tangu yalipoanza Alhamisi. Wanajeshi waliwashambulia waandamanaji waliokuwa wakirusha mawe na mabomu ya petroli barabarani, baada ya wanajeshi kusonga mbele katika eneo la kibiashara la Rath Chap Rasong. Wanajeshi hao wamelivamia eneo hilo kwa azma ya kuzima maandamano ya upinzani yanayoendelea tangu miezi miwili hivi sasa. Waandamanaji hao wanaipinga serikali ya Waziri Mkuu Abhist Vejjajiva. Barabara zinazoelekea katika eneo la biashara zimefungwa, ili kuzuia waandamanaji kuingia katika maeneo hayo. Hali ya hatari imetangazwa katika maeneo mengi nchini humo ikiwa ni pamoja na mji mkuu Bangkok.

Mwandishi:Munira Muhammad/IPS

IMhariri:P.Martin