1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Magazetini.

Mtullya, Abdu Said2 Septemba 2008

Katika maoni yao wahariri wa magazeti ya Ujerumani leo wanazungumzia hasa juu ya mkutano maalumu wa viongozi wa Umoja wa Ulaya juu ya mgogoro wa Georgia.

https://p.dw.com/p/F9lw
Rais Sarkozy wa Ufaransa kwenye kikao cha dharura cha viongozi wa Umoja wa Ulaya mjini Brussels.Picha: AP

 Wahariri  wa  magazeti  ya  Ujerumani karibu yote  leo wanazungumzia  juu  ya mkutano maalumu  wa viongozi wa nchi za Umoja wa Ulaya kuhusu mogogoro wa  Georgia  uliofanyika  jana  mjini Brussels....

Lakini wahariri hao  pia wamezungumzia juu ya hatua   ya benki ya  Commerz  kuinunua  benki  ya Dresdener. Wahariri  wa magazeti  pia hawakusahau  kutoa maoni  yao juu  ya mkutano  mkuu  wa  chama  cha Republican  nchini Marekani.

Juu ya kikao maalumu cha viongozi wa nchi za Umoja  wa Ulaya gazeti la Lausitzer Rundschau linasema   jambo muhimu  ni kwamba kikao hicho kilifikia lengo  lake-  yaani  kuzungumza kwa kauli moja. Lakini mhariri wa gazeti hilo anasema ,kuzungumza kwa sauti moja tu  hakutoshi. Kinachotakiwa  ni kuzungumza  kwa kauli ya uwazi.  Hatua ya kijeshi iliyochukuliwa na  Georgia, haikuwa ya busara na   ilisababisha  vita.

Kwa hiyo, sasa ikiwa Georgia inataka kusaidiwa na  nchi za Umoja wa Ulaya inapaswa kufuata shabaha zinazolengwa na Umoja huo. Aidha mhariri wa Lausitizer  Rundschau anautaka Umoja wa Ulaya  utoe kauli ya uwazi kwa wahusika wengine, na hasa Marekani,  kwamba nayo pia inapaswa kutimiza wajibu wake. Lakini  gazeti  la Offenburger   Tageblatt  linasema Umoja wa Ulaya unadhibitiwa  na maslahi ya kila mwanachama  binafsi. Na matokeo  yake  ni  maafikiano  ya upeo wa  chini katika ngazi  ya kimataifa.

Gazeti la Westfalen Post linatoa maoni juu ya hatua  ya benki ya  Commerz kuinunua  benki  ya Dresdener. Mhariri wa gazeti  hilo analalamika  kuwa  hatua hiyo  itateketeza nafasi za ajira  alfu sita na  mia tano nchini Ujerumani pekee, na matawi ya benki 350 yatafungwa.

Lakina katika upande mwingine gazeti la Rhein Zeitung linafurahi kwamba benki ya Dresdener  imenunuliwa na benki  ya Commerz,  badala ya kumezwa na benki ya serikali ya China.


Mhariri wa gazeti la  Frankfurter Rundschau   anaesema  ,kwamba kwa kujaribu kuweka kando  maslahi yake ,ili kushikamana na watu wanaokabiliwa  na madhara ya  kimbunga Gustav,  chama cha  Republican  asilani hakijiongezei sifa, kutokana na utobwe  alionesha  rais Bush,  wakati  wa  kimbunga  Katrina.


Conclusion...