1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Majeshi ya nchi za Kiafrika yatakuwa pekee kuweka amani Darfur nchini Sudan

14 Agosti 2007

Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika, AU, Alpha Oumar Konare, amesema majeshi ya nchi za Kiafrika yatakuwa pekee ndani ya jeshi la askari 26,000 la kuweka amani katika mkoa wa michafuko wa Darfur nchini Sudan.

https://p.dw.com/p/CH9g
Wakimbizi kwenye mkoa wa machafuko wa Darfur,Sudan
Wakimbizi kwenye mkoa wa machafuko wa Darfur,SudanPicha: AP

Amesema kumetolewa ahadi za kutosha kutoka nchi za Kiafrika kutaka kuchangia sehemu kubwa sana ya jeshi hilo la mchanganyiko ambalo limekubaliwa na Umoja wa Mataifa wiki iliopita. Alisema mpira sasa uko upande wa Umoja wa Mataifa kutoa kwa haraka fedha zinazohitajiwa kwa ajili ya operesheni hiyo. Umoja wa Mataifa ulipendekeza kuweko jeshi la mchanganyiko kutoka Umoja wa Afrika na Umoja wa Mstaifa kama njia ya kumshawishi Rais wa Sudan, Omar al-Bashir,aruhusu wanajeshi wa kutoka ngambo, ambao yeye alisema hapo mwanzoni kuwa ni sawa na kuukaribisha ukoloni mambo leo.

Othman Miraji alizungumza na Profesa Samuel Mushi wa taaluma za siasa katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kumuuliza kauli hiyo ya Bwana Konare ina maanisha nini.