Maharage yanayochipua sio chanzo cha E.coli
7 Juni 2011Matangazo
Wizara ya kilimo katika jimbo la Lower Saxony imeeleza kuwa karibu vipimo dazeni mbili vilivyochukuliwa kwenye shamba lililokuwa likishukiwa vimeonyesha kuwa shamba hilo sio chanzo cha kuripuka bakteria hao.
Uchunguzi katika maharage yanayochipua unaendelea, lakini Reinhard Burger, mkurugenzi wa Taasisi ya Robert Koch amesema uchunguzi wa chanzo cha bakteria hao unaweza usimalizike. Mripuko wa bakteria wa E.coli nchini Ujerumani umewaua kiasi watu 22 na zaidi ya wengine 2,300 barani Ulaya wameambukizwa.
Mawaziri wa kilimo wa Umoja wa Ulaya wanatarajiwa kukutana leo kujadiliana kuhusu usalama wa chakula na athari za kiuchumi zilizosababishwa na kitisho hicho, wakati ambapo wanunuzi wana hofu ya kununua mboga mboga kutoka Ulaya.