1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mabao 37 yatinga wavuni wiki ya kwanza Bundesliga

12 Agosti 2013

Wiki ya kwanza ya Bundesliga mabao 37 yatinga wavuni, Eintracht Frankfurt yaadhibiwa na Hertha BSC Berlin timu iliyorejea msimu huu katika daraja la kwanza la Bundesliga. Bayern Munich na Dortmund zang'ara .

https://p.dw.com/p/19OFr
Bildnummer: 13893487 Datum: 28.06.2013 Copyright: imago/MIS 28.06.2013, Fussball 2.Bundesliga 2013/2014, 1860 München im Trainingslager in Tirol, Training am Nachmittag. Der Spielball Adidas Torfabrik; GER 2014 xas x2x 2013 quer Fussball Soccer Football Herren Männer Fußball Deutschland 2.Liga Liga2 Saison 2013 / 2014 13/14 saison1213 2013/14. o0 Objekte Equipment Ligaball Ball Ausrüster Sportausrüster Hersteller Sportartikelhersteller Sportartikel Wirtschaft Perspektive Durchblick Netz Tornetz Image number 13893487 date 28 06 2013 Copyright imago MIS 28 06 2013 Football 2 Bundesliga 2013 2014 1860 Munich in Training camps in Tyrol Training at Afternoon the Play ball adidas Torfabrik ger 2014 xas x2x 2013 horizontal Football Soccer Football men Men Football Germany 2 League Season 2013 2014 13 14 2013 14 o0 Objects Equipment League ball Ball Equipment Sports equipment Manufacturers Sporting goods manufacturers Sporting goods Economy Perspective With glance Network Tor network
Nyavu zimetikisika mara 37 katika siku ya kwanza ya BundesligaPicha: imago sportfotodienst

Mchezo wa kwanza wa msimu wa 51 katika Bundesliga , mashabiki wameshuhudia mabao 37 yakitinga wavuni. Schalke 04 na Hamburg SV zilitoshana sare ya mabo 3-3 jana Jumapili(11.08.2013).

Mainz 05 ilipata ushindi katika mchezo mwingine jana dhidi ya VFB Stuttgart wa mabao 3-2.

Schalke's Austrian defender Christian Fuchs and Hamburg's defender Dennis Diekmeier (R) vie for the ball during the German first division Bundesliga football match FC Schalke 04 vs Hamburger SV in the German city of Gelsenkirchen on August 11, 2013. AFP PHOTO / PATRIK STOLLARZ RESTRICTIONS - DFL RULES TO LIMIT THE ONLINE USAGE DURING MATCH TIME TO 15 PICTURES PER MATCH. FOR FURTHER QUERIES PLEASE CONTACT DFL DIRECTLY AT + 49 69 650050. (Photo credit should read PATRIK STOLLARZ/AFP/Getty Images)
Mpambano kati ya Schalke - HamburgPicha: P.Stollarz/AFP/GettyImages

Mabingwa wapeta

Mabingwa watetezi Bayern Munich walipata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Borussia Moenchengladbach ambapo mabingwa hao walipata penalti mbili katika kipindi cha dakika 1.30. Mlinda mlango wa mabingwa hao watetezi manuel Neuer amesema wameridhika na mchezo wao.

"Tumeridhika. tumepata mabao mawili yakuongoza na mapema. Na kisha tukajifunga bao wenyewe kupitia Dante. tumepoteza hata hivyo nafasi nyingi za kufunga mabao. Lakini kwa jumla tuliweza kuthibiti kila kitu na yalikuwa matokeo mazuri".

(L-R) Bayern Munich's French midfielder Franck Ribery, Dutch midfielder Arjen Robben, striker Thomas Mueller and Croatian striker Mario Mandzukic celebrate after the second goal for Munich during the German first division Bundesliga football match FC Bayern Munich vs Borussia Moenchengladbach in Munich, southern Germany on August 9, 2013. AFP PHOTO / CHRISTOF STACHE RESTRICTIONS - DFL RULES TO LIMIT THE ONLINE USAGE DURING MATCH TIME TO 15 PICTURES PER MATCH. FOR FURTHER QUERIES PLEASE CONTACT DFL DIRECTLY AT + 49 69 650050. (Photo credit should read CHRISTOF STACHE/AFP/Getty Images)
Wachezaji wa Bayern München wakisherehekea baoPicha: Christof Stache/AFP/Getty Images

Nao makamu bingwa Borussia Dortmund ilizoa point tatu zote kwa ushindi wa kishindo wa mabao 4-0 dhidi ya FC Augsburg , na mshambuliaji Aubameyang akianza Bundesliga kwa kishindo kwa kupachika mabao 3.Mlinzi wa Dortmund Neven Subotic alimwagia sifa mshambuliaji wa timu hiyo Aubameyang.

"Ni kitu cha kipekee kwa Aubameyang , ulikuwa mchezo wa aina yake. Matokeo ya mchezo huo pamoja na mabao aliyofunga , amefanya kazi nzuri sana na tulimsaidia vizuri kutimiza hilo. Tulicheza vizuri na kupambana kwa kiwango cha juu na tulistahili kushinda".

AUGSBURG, GERMANY - AUGUST 10: Pierre-Emerick Aubameyang of Dortmund celebrates his second goal during the Bundesliga match between FC Augsburg and Borussia Dortmund at SGL Arena on August 10, 2013 in Augsburg, Germany. (Photo by Lennart Preiss/Bongarts/Getty Images)
Pierre-Emerick Aubameyang akisherehekea moja kati ya mabao yake matatu dhidi ya AugsburgPicha: Getty Images

Kipigo cha mbwa mwizi

Katika mchezo huo wa wiki ya kwanza ya Bundesliga , timu iliyorejea katika daraja la kwanza msimu huu Hertha BSC Berlin inashikilia usukani kwa kutumbukiza wavuni mabao mengi, ambapo iliisambaratisha Eintracht Frankfurt kwa mabao 6-1 na kumshangaza hata kocha wao Jos Luhukay. Kama anavyosema mchezaji wa kiungo wa Hertha john Brooks.

"Tumeuchukulia ushindi huu kwa unyenyekevu. Kwasababu umetufanya tujisikia furaha, si jambo la kawaida. Si kila wiki timu inaweza kushinda mabao 6-1. Kwetu sisi ni mafanikio makubwa kwa kuanza msimu. Kwa mashabiki wetu wakituunga mkono ilikuwa furaha kubwa. Wanaposema wiki ijayo tuendelee kufanya hivyo , naungana nao moja kwa moja".

CAPTION CORRECTION - Corrects players name Hertha's defender John Anthony Brooks celebrates after scoring during the German first division Bundesliga match Hertha Berlin vs Eintracht Frankfurt in Berlin, on August 10, 2013. AFP PHOTO/ JOHN MACDOUGALL RESTRICTIONS - DFL RULES TO LIMIT THE ONLINE USAGE DURING MATCH TIME TO 15 PICTURES PER MATCH. FOR FURTHER QUERIES PLEASE CONTACT DFL DIRECTLY AT + 49 69 650050. (Photo credit should read JOHN MACDOUGALL/AFP/Getty Images)
Hertha BSC Berlin waifanyia kitu mbaya Eintracht FrankfurtPicha: J.Macdougall/AFP/GettyImages

Michezo ya kirafiki

Wakati huo huo Bundesliga inapumzika kwa wiki moja kupisha michezo ya kirafiki ya kimataifa ya timu ya taifa. Ujerumani inapambana na Paraguay.

Michezo hiyo ya kirafiki ya kimataifa katika bara la Ulaya na kwingineko inaashiria mwanzo wa msimu ambao fainali za kombe la dunia mwaka ujao nchini Brazil zinakaribia.

Baadhi ya vigogo vya soka barani Ulaya vinapambana wenyewe kwa wenyewe wakati kuna mapambano kadha kati ya timu za bara la Ulaya dhidi ya timu kutoka bara la America ya kusini.

Mabingwa wa dunia Uhispania wanasafiri kwenda Ecuador, wakati Italia inatiana kifuani na Argentina na Ujerumani ina miadi na Paraguay.

Timu za mataifa kadha ya America ya kusini zimeamua kupambana na ama mataifa ya Ulaya ama ya Asia , ikiwa ni pamoja na wenyeji wa fainali za kombe la dunia Brazil ambayo inakibarua dhidi ya Uswisi mjini Basel.

Kwingineko Colombia inakutana na Serbia mjini Barcelona , Uruguay inapimana nguvu na Japan, Peru ikipima uwezo wake dhidi ya Korea ya kusini na Chile inakutana na Iraq nchini Denmark.

kuna mapambano yanayovuta hisia , wakati Uingereza ikipima kiwango cha uhasama kilichopo kati yake na Scotland, Ureno ikiikaribisha Uholanzi, na Ubelgiji dhidi ya Ufaransa na Sweden inapimana nguvu na ndugu zao wa Denmark.

Wakati huo huo mchezaji nyota chipukizi Julian Draxler hataweza kujiunga na wenzake katika kikosi cha timu ya taifa ya Ujerumani ambacho kitakuwa uwanjani siku ya Jumatano kupambana na Paraguay baada ya kuumia mguu katika mchezo wa ufunguzi wa Bundesliga, limesema shirikisho la kandanda la Ujerumani DFB leo.

Chipukizi huyo mwenye umri wa miaka 19 mchezaji wa kati wa Schalke 04 amepata maumivu hayo katika mchezo kati ya timu yake na Hamburg SV jana Jumapili.

A doctor looks at an injury of Schalke 04's Julian Draxler (L) during the German first division Bundesliga soccer match against Hamburg SV in Gelsenkirchen August 11, 2013. REUTERS/Ina Fassbender (GERMANY - Tags: SPORT SOCCER HEALTH) DFL RULES TO LIMIT THE ONLINE USAGE DURING MATCH TIME TO 15 PICTURES PER GAME. IMAGE SEQUENCES TO SIMULATE VIDEO IS NOT ALLOWED AT ANY TIME. FOR FURTHER QUERIES PLEASE CONTACT DFL DIRECTLY AT + 49 69 650050
Mchezaji wa Schalke 04Julian Draxler akipatiwa matibabuPicha: Reuters

Ujerumani inashikilia nafasi ya kwanza katika kundi lake la kufuzu kucheza fainali za kombe la dunia ikiwa na points 16 , point sita mbele ya Austria, ambayo inapambana nayo hapo Septemba 6 kabla ya kwenda katika visiwa vya Faroe siku nne baadaye. Sweden na Ireland katika kundi hilo zina points 11 kila moja.

Gabon kwenda Afrika kusini

Katika bara la Afrika Gabon imefanikiwa kufuzu kucheza fainali za kombe la Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani , baada ya kuipa kipigo Cameroon cha bao 1-0. Katika mchezo wa kwanza Cameroon ilipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Gabon. Gabon ilishinda kwa mikwaju ya penalti 6-5 na kufuzu kuingia katika fainali hizo baada ya kutoka sare katika matokeo jumla kwa bao 1-1.

Gabon imefuzu kucheza katika fainali hizo zitakazofanyika Januari 11 nchini Afrika kusini na Cameroon sasa itapambana na jamhuri ya kidemokrasi ya Congo wakiwania nafasi nyingine katika fainali hizo. Mchezo kati ya Zimbabwe na Zambia umeahirishwa hadi Agosti 18 na pia mchezo kati ya Msumbiji na Angola umeahirishwa hadi Agosti 25.

Usain Bolt

MOSCOW, RUSSIA - AUGUST 11: Usain Bolt of Jamaica celebrates winning gold in the Men's 100 metres Final during Day Two of the 14th IAAF World Athletics Championships Moscow 2013 at Luzhniki Stadium on August 11, 2013 in Moscow, Russia. (Photo by Paul Gilham/Getty Images)
Bingwa wa dunia wa mita 100 Usain BoltPicha: Getty Images

Mashindano ya ubingwa wa dunia wa Riadha yanaendelea mjini Moscow , ambapo jana(11.08.2013) mkimbiaji mbio fupi Usain Bolt aliwahakikishia mashabiki wake kuwa bado ni moto wa kuotea kwa mbali pale aliposhinda mbio za mita 100 kwa kutumia sekunde 9.77.

Mwandishi: Sekione Kitojo / dpae / rtre / ZR

Mhariri: Yusuf Saumu