1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Maandamano makubwa Cairo baada ya mswada kuidhinishwa

1 Desemba 2012

Mamia kwa maelfu ya waandamanaji waliingia mitaani mjini Cairo Ijumaa(30.11.2012) kuongeza mbinyo kwa rais Morsi baada ya jopo lenye wajumbe wengi kutoka kundi la Kiislamu kupitisha mswada wa katiba wa nchi hiyo.

https://p.dw.com/p/16tzm
Tens of thousands of protesters gather in Egypt's landmark Tahrir square against a decree by President Mohamed Morsi granting himself broad powers that shield his decisions from judicial review on November 30, 2012 in Cairo. Activists were are rallying a day after a Islamist-dominated panel rushed through a draft constitution, escalating the political stand-off between Morsi and his opposition. AFP PHOTO/GIANLUIGI GUERCIA (Photo credit should read GIANLUIGI GUERCIA/AFP/Getty Images)
Waandamanaji katika uwanja wa Tahir mjini CairoPicha: Gianluigi Guercia/AFP/Getty Images

Katiba hiyo mpya , ambayo imeidhinishwa baada ya vikao virefu usiku wa jana na ambayo imesusiwa na wajumbe wenye msimamo wa kati na Wakristo, inazua wasi wasi mkubwa kuhusu masuala ya haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na uhuru wa kidini, wanasema wanaharakati.

Morsi atapitia upya mswada huo leo Jumamosi,(01.12.2012), amesema spika wa bunge Hossam el-Ghiriani, na anatarajiwa baadaye kuitisha kura ya maoni katika muda wa wiki mbili.

GettyImages 157156665 Members of Egypt's constituent assembly discuss of the last voting session on a new draft constitution at the Shoura Assembly on November 29, 2012 in Cairo. The assembly retained today the principles of Islamic law as the main source of law, as it rushed through the approval process over objections from an opposition that argues more time is needed. It also agreed a clause stating that the principles of Christian and Jewish legal traditions would guide the personal and religious affairs of people belonging to those faiths. The vote comes amid accusations that the Islamist-dominated panel is railroading the charter through and protests over President Mohamed Morsi's assumption of sweeping powers, which has plunged the country into its worse crisis since Morsi took office in June. AFP PHOTO / GIANLUIGI GUERCIA (Photo credit should read GIANLUIGI GUERCIA/AFP/Getty Images)
Wajumbe wa baraza la kutunga katiba wakiidhinisha mswada huoPicha: AFP/Getty Images

Katiba hiyo imechukua nafasi ya kati katika mzozo mbaya kabisa wa kisiasa nchini humo tangu pale Morsi alipochaguliwa mwezi Juni mwaka huu, ukiyahusisha kwa kiasi kikubwa makundi ya Kiislamu na wapinzani kutoka makundi yenye misimamo ya wastani.

"Iilaaniwe bunge la katiba," kundi kubwa ambalo lilikuwa na vipaaza sauti liliimba wakati wakiingia katika uwanja wa Tahrir, eneo lililotumika katika vuguvugu ambalo liliuondoa madarakani hatimaye utawala wa rais Hosni Mubarak mapema mwaka 2011.

Mabango yakimshutumu "Morsi kuwa ni dikteta" wakati waandamanaji wakipaaza sauti "Ulaaniwe utawala wa kiongozi," wakiwa na maana ya kiongozi wa chama cha udugu wa Kiislamu, ambapo Morsi alijitokeza kupitia chama hicho kabla ya kuwa rais.

FILE - In this Friday, July 13, 2012 file photo, Egyptian President Mohammed Morsi speaks to reporters during a joint news conference with Tunisian President Moncef Marzouki, unseen, at the Presidential palace in Cairo, Egypt. Egypt’s Islamist president may hail from the fiercely anti-Israeli Muslim Brotherhood, but in his first major crisis over Israel, he is behaving much like his predecessor, Hosni Mubarak:. He recalled the ambassador and engaged in empty rhetoric supporting Palestinians. Mohammed Morsi is under pressure at home to do more but he is just as wary as Mubarak about straining ties with the United States. (Foto:Maya Alleruzzo, File/AP/dapd)
Rais wa Misri Mohammed MursiPicha: AP

Maandamano msikitini

Maandanano mengine yalizuka wakati Morsi alipokuwa akisali katika msikiti mjini Cairo, baada ya imam kuwataka Waislamu kumuunga mkono rais, lakini hakukuwa na tukio kubwa.

Mapambano yalizuka katika mji wa kaskazini wa Alexandria baina ya waandamanaji wanaomuunga mkono na rais Morsi na wale wanaompinga, duru za usalama zimesema , lakini hakukupatikana taarifa mara moja za watu waliojeruhiwa. Maandamano yanatarajiwa kufanywa na kambi zote mjini Cairo leo Jumamosi(01.12.2012).

Mzozo wa hivi sasa ulizuka baada ya rais Morsi kutoa tamko hapo Novemba 22 akijipa madaraka makubwa na kuwezesha uamuzi wake wowote kutopingwa na mahakama, hali ambayo ilizusha maandamano pamoja na mgomo wa majaji.

epa03488884 Vice President of the Egyptian Supreme Constitutional Court, Maher Sami, speaks during a press conference at the court_s headquarters in Cairo, Egypt, 28 November 2012. Egypt's top court on 28 November accused President Mohamed Morsi of hurting its image by claiming that its decision in June to invalidate the Islamist-led lower house of parliament was biased. EPA/KHALED ELFIQI +++(c) dpa - Bildfunk+++
Rais wa mahakama kuu ya katiba Maher Sami mjini CairoPicha: picture alliance / dpa

Katiba mpya huenda isipitishwe

Amri aliyotoa imezuwia chombo kikuu cha sheria , mahakama ya katiba kuwa na uwezo wa kulivunja bunge linaloongozwa na kundi la Waislamu , katika uamuzi ambao wangeuchukua siku ya Jumapili kuhusu uhalali wa kisheria wa bunge hilo la katiba.

Bunge la katiba limeandika mswada wa katiba ambao utachukua nafasi ya katiba ya zamani ambayo imesitishwa baada ya kuondolewa madarakani kwa rais Hosni Mubarak mwaka jana , lakini kukamilishwa kwake kumesogezwa mbele kutokana na mtafaruku uliosababishwa na amri aliyoitoa rais Morsi.

Egyptian security forces, background, clash with protesters near Tahrir Square in Cairo, Egypt, Sunday, Nov. 25, 2012. Supporters and opponents of Egypt's president grow more entrenched in their potentially destabilizing battle over the Islamist leader's move to give himself near absolute powers, with neither side appearing willing to back down. (Foto:Ahmed Gomaa/AP/dapd)
Maandamano yenye ghasia mjini CairoPicha: AP

Mgomo wa majaji uliotishwa na mahakama ya katiba pamoja na mahakama nyingine kunaweza kuiweka hatua ya kura ya maoni katika hatari, iwapo majaji ambao kwa kawaida hufanya uchunguzi wa uchaguzi watakataa kuipa kura hiyo uhalali.

Wanaharakati wameushambulia mswada huo wa katiba , wakisema unalinda baadhi ya sheria kwa kukandamiza nyingine.

Mwandishi: Sekione Kitojo /afpe
Mhariri: Iddi Ssessanga