1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

LONDON: Ugonjwa wa miguu na midomo umetokea maabara

13 Septemba 2007
https://p.dw.com/p/CBQ5

Maafisa nchini Uingereza wamesema,ugonjwa wa miguu na midomo ulioripuka hivi karibuni nchini humo ni sawa na ule uliotokea mwezi uliopita. Wakulima walikuwa na wasiwasi kuwa virusi vya aina mpya vitawalazimu kuua mifugo yao.Ugonjwa wa ulioripuka mwezi uliopita kwenye shamba la mifugo katika eneo la Surrey,ulihusishwa na maabara ya jirani.