LISBON: Rais Putin tayari kwa mazungumzo na Umoja wa Ulaya
25 Oktoba 2007Matangazo
Rais Vladimir Putin wa Urusi leo anatarajiwa kuwasili mjini Lisbon ambapo atafanya mazungumzo na viongozi wa Ureno kabla ya mkutano wake na viongozi wa Umoja wa Ulaya hapo kesho .
Wadadisi wamesema mkutano huo unaweza kukabiliwa na mvutano juu ya masuala ya nishati na biashara.
Rais Putin anaetarajiwa kuwasili Ureno leo alasiri,atakutana na rais Anibal Silva pamoja waziri mkuu wa nchi hiyo Jose Socrates.