1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

KINSHASA:Rais Kabila afanyia mabadiliko jeshi lake

13 Juni 2007
https://p.dw.com/p/CBs1

Rais Joseph Kabila amefanya mabadiliko katika uongozi wa jeshi lake.

Kwa mujibu wa ripoti zilizotangazwa na televiesheni ya taifa mjini Kinshasa rais Kabila amemteua Luteni generali Diedonne Kayembe Mbandakulu kuwa mkuu wa majeshi yote akichukua mahala pa luteni generali Philemon Kisempia Sungilanga.

Wataalamu wanasema orodha hiyo mpya jeshini inawajumuisha wale waliowatiifu kwa rais Kabila.

Bwana Diodonne mwenye umri wa miaka 6122 ni mzaliwa wa kusini mashariki mwa jimbo la Katanga ngome ya familia ya rais Kabila.