KINSHASA: Watu 14 wauwawa mashariki mwa Kongo
3 Oktoba 2006Matangazo
Watu takriban 14 wameuwawa katika mapigano yaliyotokea mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Afisa wa Umoja wa Mataifa katika eneo hilo amesema waliouwawa ni wanamgambo 12 na wanajeshi wawili wa Kongo.
Msemaji wa umoja wa Mataifa mjini Bunia, Leocadio Salmeron, amesema mapigano yalizuka mnamo Jumapili iliyopita katika kijiji cha Singo, yapata kilomita 60 kusini mwa Bunia.
Jeshi la Kongo limeiambia tume ya Umoja wa Mataifa mjini Bunia kwamba wanajeshi wake saba wamejeruhiwa katika mapiganao hayo.