1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Khartoum.Muungano wa mahakama za kiislamu wakataa mazungumzo.

31 Oktoba 2006
https://p.dw.com/p/CCxU

Muungano wa mahakama za kiislamu wenye nguvu nchini Somalia hii leo umekataa kushiriki katika mazungumzo ya amani pamoja na serikali ya mpito ya nchi hiyo.

Viongozi wa kiislamu mjini Mogadishu wamesema kwamba mazungumzo hayawezi kuendelea hadi vikosi vya kijeshi vya Umoja wa Ulaya vitakapoondoshwa nchini Somalia na hadi Kenya itakapojumuishwa kama mpatanishi mwenza katika mazungumzo hayo.

Ujumbe wa waislamu ukizungumza na shirika la habari la Ufaransa AFP wamesisitiza msimamo wao wa kutoshiriki mazungumzo hayo hadi matakwa yao mawili yatakapotimizwa.

Nao ujumbe wa serikali ya Somalia uliowasili Khartoum tangu jana umesema kuwa, hautakubali masharti yaliyotolewa na upande wa pili, jambo ambalo bado linazusha khofu ya kuendelea na vita katika nchi hiyo.