KAMPALA : Wawili wauawawa kwenye mripuko wa gari
17 Februari 2007Matangazo
Watu wawili wameuwawa wakati gari lao liliporipuka kwenye viunga vya mji mkuu wa Kampala hapo jana usiku.
Msemaji wa polisi wa Uganda Judith Nabakoba amesema watu wawili imetihibitika kuwa wameuwawa na kwamba inaonekana kuwa kulikuwako na mripuko ndani ya gari hilo ambalo lilikuwa ni gari la raia.
Mkuu wa polisi wa Kampala Grace Turyagumanawe amesema kwa hakika huo ulikuwa ni mripuko lakini hawezi kutowa maelezo zaidi kwa sasa.Pia amesema kulikuwa na watu wengine ndani ya gari hilo waliofikishwa hospitali lakini hakusema wamejeruhiwa kwa kiasi gani au ni wangapi.