JOHANNESBURG: Mpango wa matibabu wakosolewa na Tutu
1 Septemba 2007Matangazo
Askofu Mkuu Desmond Tutu,ameishambulia vikali serikali ya Afrika Kusini kuhusu kucheleweshwa kwa kuanzishwa mpango wa matibabu ya virusi vya HIV na UKIMWI nchini humo.Amesema,maoni ya imani isio sahihi ya viongozi wa nchi hiyo, yamesababisha vifo ambavyo vingeweza kuzuilika.