1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

JERUSALEM:Shimon Peres achaguliwa rais wa Israel

13 Juni 2007
https://p.dw.com/p/CBs4

Mwanasiasa mkongwe wa Israel Shimon Peres amechaguliwa kuwa rais mpya wa taifa hilo baada ya kujizolea kura 86 za wabunge 120

Peres amepata ushindi katika duru ya pili ya uchaguzi kufuatia kujiondoa kwenye kinyanga’nyiro hicho wapinzani wake wawili.

Punde tu baada ya kutangazwa mshindi Peres alizungumzia suala la amani na wapalestina akisema.

Kila mmoja anachagua kiongozi wake wapalestina wanachagua viongozi wao na waisrael vile vile lakini hakuna anaweza kuishi bila amani kwa hivyo inabidi tukae na tujadiliane.

Peres mwenye umri wa miaka 83 anachukua wadhifa war ais unaoshikiliwa na Moshe Katsav ambaye anakabiliwa na kashfa ya kumbaka mwanamke.