1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

JEDDAH: Rais Abbas azuru Saudi Arabia

12 Septemba 2007
https://p.dw.com/p/CBQe

Rais wa mamlaka ya Palestina, Mahmoud Abbas, amesema amezungumza na mfalme wa Saudi Arabia juu ya mkutano wa kimataifa kuhusu amani ya mashariki ya kati na hali ya kisiasa katika maeneo ya Wapalestina.

Rais Abbas amefutilia mbali uwezekano wa kufanya mazungumzo na kundi la Hamas mpaka litakapourejesha ukanda wa Gaza katika utawala wa mamlaka ya Palestina.

Rais Abbas ambaye ameondoka mjini Jedda kuelekea Amman Jordan, amesema atakutana na mfalme Abdullah II wa Jordan hii leo.