1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

JAKARTA: Manusura 15 wa ajali ya feri waokolewa

8 Januari 2007
https://p.dw.com/p/CCcS

Manusura 15 wa ajali ya feri iliyotokea nchini Indonesia waliokolewa jana jioni baada ya kuelea majini kwa siku tisa. Afisa wa uokozi amesema mmoja wa manusura hao alifariki dunia muda mfupi baada ya kuokolewa na meli ya mizigo.

Operesheni ya kuwatafuta mamia ya manusura wengine wasiojulikana waliko mpaka sasa baada ya feri walimokuwa wakisafiria kuzama katika pwani ya kisiwa cha Java mnamo Disemba 29 mwaka jana, itapanuliwa.

Wakati haya yakiarifiwa, maofisa nchini Indonesia wanaendelea kuitafuta ndege ya abiria iliyopotea kufuatia hali mbaya ya hewa wiki moja iliyopita. Juhudi za kuitafuta ndege hiyo zinafanyika kisiwani Sulawesi na maeneo ya pwani ya kisiwa hicho.