1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

ISLAMABAD:aachiwa bila ya mashtaka baada ya mahabusu ya miaka mitatu

21 Agosti 2007
https://p.dw.com/p/CBXG

Pakistan imemwachia bila ya mashtaka mtaalamu wa kompyuta alietuhumiwa kuwa na uhusiano na mtandao wa kigaidi wa al-Kaida, baada ya kumweka mahabusu kwa muda wa miaka mitatu. Mtaalamu huyo Mohammed Noor Khan alidaiwa kuwa kiunganishi baina ya viongozi wa al-Kaida na wapiganaji wa mtandao huo.