1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Iran yakanusha silaha za nuklia

9 Desemba 2007

---

https://p.dw.com/p/CZPs

TEHERAN:

Msemaji wa wizara ya nje ya Iran, leo amekanusha madai ya mashirika ya ujasusi ya kimarekani kuwa Iran ilikua na mradi wa kuunda silaha za kinuklia kabla ya mwaka 2003.

„Iran haikuwa na mradi wa silaha za kinuklia wakati wowote-sio kabla 2003 wala baadae na madai yoyote yasemayo hivyo hayana msingi wowote.“

Kutokana na ripoti ya mashirika 16 ya ujasusi ya Marekani kukanusha Iran haikuwa na mradi wa silaha za kinuklia baada ya 2003, Iran imeanza kudai kwamba nchi za magharibi zikome kutoa mashtaka yoyote ya aina hiyo dhidi ya Iran na haioni uhalali wowote wa kupitishwa azimio jengine la UM kudai iwekewe vikwazo vya fedha.