Mashirika ya kutetea haki za kibinadamu nchini Tanzania yamesema kuwa jeshi la polisi limetumia nguvu kupita kiasi katika kushughulikia walemavu waliokuwa wakifanya maandamano kupinga amri ya kutofika katikati ya mji wakisafirisha abiria kwa kutumia pikipiki zao za miguu mitatu zijulikanazo kama bajaji. Sikiliza ripoti ya Hawa Bihoga.