GAZA: Mashambulizi ya Israel yameua wanamgambo 10
6 Julai 2007Matangazo
Hadi Wapalestina 10 wameuawa baada ya vikosi na vifaru vya Israel kuingia katikati ya Ukanda wa Gaza.Katika mapambano yaliyozuka kwenye kambi ya wakimbizi ya al-Maghazi,risasi zilifyatuliwa kati ya majeshi ya Israel na wanamgambo wa Kipalestina.Kwa mujibu wa duru za hospitali,watu wengine 13 pia walijeruhiwa katika mapambano hayo.