GAZA CITY: Ismail Haniyeh apona chupu chupu
21 Oktoba 2006Matangazo
Waziri mkuu wa Wapalestina Ismail Haniyeh wa chama cha Hamas,amepona chupu chupu baada ya kushambuliwa katika Ukanda wa Gaza.Kwa mujibu wa Hamas,watu wasiojulikana walifyatulia risasi mlolongo wa magari ya waziri mkuu.Vikosi vya usalama vya Hamas vilimkinga Haniyeh.Wizara ya mambo ya ndani ya Wapalestina,imesema shambulio hilo limefanywa na ukoo fulani.