1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mtandao wa intaneti na simu vyafungiwa

Sekione Kitojo
1 Desemba 2016

Gambia leo imefanya uchaguzi wa rais ambapo rais aliyeko madarakani Yahya Jammeh anakabiliwa na upinzani mkubwa kwa mara ya kwanza

https://p.dw.com/p/2TaPA
Elfenbeinküste Präsident Yahya Jammeh in Yamoussoukro
Picha: Getty Images/AFP/I. Sanogo

Gambia imefunga mtandao wa intaneti na simu katika taifa hilo dogo la Afrika magharibi leo, wakati  upigaji kura katika uchaguzi  wa  rais ukianza nchini humo.

Kufungwa kwa mitandao na mawasiliano ya simu , na watoaji  huduma za intaneti ambako kunayaathiri makampuni yanayomilikiwa  na serikali na pia makampuni ya binafsi, kunakuja wakati  utawala wa rais Yahya Jammeh wa miaka 22 unakabiliwa na upinzani mkubwa kwa mara ya kwanza.

Kanali huyo wa zamani wa jeshi, ambaye aliingia madarakani katika mapinduzi ya mwaka 1994 na analitawala taifa hilo kwa mkono  wa chuma, anawania kipindi cha tano dhidi ya wagombea wengine wawili.

Mpizani wake mkubwa Adama Barrow, anaungwa mkono na vyama saba vya upinzani na ni maarufu akikubalika na vijana wengi  wa nchi hiyo ambao hawana ajira. Mfanyabiashara huyo anaahidi kurejesha demokrasia na utawala wa sheria na kuwaacha huru  wafungwa wote wa kisiasa.