1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Frankfurt: Bei za hisa za makampuni duniani zimeanguka hapo jana.

28 Februari 2007
https://p.dw.com/p/CCNy

Bei za hisa za makampuni zilianguka duniani kote hapo jana baada ya kuanguka kwa asilimia tisa huko Uchina. Hicho ni kiwango kikubwa kabisa cha kwenda chini hisa kushuhudiwa mnamo mwongo mmoja uliopita. Baada ya kupita wiki ya kupanda juu, bei za hisa hapa Ujerumani zilianguka kwa asilimia mbili hapo jana jioni. Pia soko la hisa la New York la Dow Jones lilishuhudia hali kama hiyo. Lakini katika biashara ya leo asubuhi, bei za hisa huko Shanghai zilipanda kwa zaidi ya asilimia moja.